Wednesday, January 11, 2012

NDOA NA WANAWAKE


Wapendwa wangu leo nataka tuongee kidogo, nimeona ni vizuri kama tutashauriana pia ili tuone kama inawezekana kufanya hivyo mikasa kwenye ndoa zetu isitokee.
Katika mikasa mingi sana inawahusisha wanandoa, hasa wanawake,  mara mume wangu nimemfumania, mara mume wangu kiburi, mara mume wangu mchafu na mengine mengi, lakini je hamuwezi ninyi kama kina mama kuangalia ni jinsi gani mnaweza kufanya ili kuzuia? na pale yanapotokea basi iwe imebidi yatokee?ila ninyi msiwe chanzo.
Mshauriane kwa pamoja, mfanye nini ili mpunguze hii kasi ya machafuko kwa wanandoa, nina amini kabisa kama kila mtu ataplay part yake kama mama mwenye hekima basi 80% ya ndoa zetu  zitakuwa zimepona.

(i) KUNUNA KUSIPITILEZE.

Kununa imo, lakini sio nongwa jamani, mtu ukinuna basi ndio lo!! Mwezi mzima, sasa tujiulize mnaponunia waume zenu mwezi mzima mnategemea nini???
Kama anakuhitaji kifamilia zaidi wewe si atapata nafasi ya kutoka nje? Maana akirudi home anaona kero, mama kanuna, tena wengine bila hata haya wanawambia watoto baba akija msimuamkie mkalale, kha! Baba lazima ajiulize hivi kuna haja gani ya kuwahi nyumbani, bora nikae bar nileweeeeeee, matokeo yake anaanza kurudi usiku amechoka baba wa watu,  na anarudi tu! kutimiza wajibu.

Pale inapobidi kukasirika,  yes! Show him kwamba hapa umekosea, ili nae ajuwe asikupande kichwani,  na kama umeamua  kumtingisha kwa kununa basi huo mnuno wako uwe na kiasi, sio ndio kila akikusemesha umevuta mdomo, jamani msipoangalia  mtazipoteza ndoa zenu wakati bado mnazitaka.

Mbali na hilo tukumbuke katika yale mambo serios lazima tuwe serios kweli, mfano kuna mmoja alisema ameambiwa aache kazi,  dada huyu anaweza kukaa namumewe kwa upole na upendo akamwambia tu! kwanini niache kazi? asikilize hizo sababu, ili nae apate muda wa kujitetea, pengine kazi inamtia kiburi anasahau majukumu yake kama mama ?
Pengine baba hapati huduma inavyostahili ? pengine housegirl ndio kila kitu ? hadi kusema hivyo lazima kuna reason, tusikimbilie kusema ondoka, au achana nae,  we! usipime, mume mtamu jamani, mume anauma asikwambie mtu, ifike kipindi mjichunguze je mna mapungufu gani ninyi kina mama kwa upande wenu, kabla hamjaanza kulaumu waume zenu.

Kinamama mnapoishi na waume zenu kwenye ndoa, baada ya muda huwa  mnajenga mazowea, ambayo sometimes yanakuwa hayajengi bali yanabomoa, mazowea ya aina hii huleta kiburi ambacho kwa namna moja ama nyingine kina madhara makubwa sana, unakuta mwanamke anamdomo mchafu afadhali ya choo, anamjibu mumewe majibu machafu hata mbele za watu /watoto wao.

Kitu ambacho ni kibaya sana, sababu wale watu wanaowazunguka ninyi wawili watajua tofauti zenu, na mtatiana aibu sana maisha yenu yatakuwa nje, kila mtu atawaona vihoja kuanzia watoto hadi majirani, lo! mbadilike jamani.

Mume anataka kuheshimiwa, ili na watoto wajifunze heshima kupitia kwa mama yao, lakini utakuta mtu akiudhiwa anaropoka hovyo maneno makali ambayo baada ya ugomvi wao kuisha inageuka kuwa aibu kwake.

ii) (MALIZENI TOFAUTI ZENU CHUMBANI KWENU )

Turejee mafundisho ambayo wengi wenu huwa mnapewa kwenye Kitchen Party zenu, malizeni chumbani migogoro yenu, au hata ukimnunia  basi watoto wasijue, au majirani, mwingine akinuna basi hata kama ni maji ya kuoga haweki, kama ni nguo ya ndani ndio hatafua tena, kama ni chakula ndio hatamuandalia tena, jamani jamani, mjitahidi jamani ndoa ni ghali.

Wanaume ni kama watoto wadogo, utakavyompenda mwanao na kumuweka karibu na wewe ndio atakupenda sana, lakini mtoto ukimfokea fokea tu atakuogopa na kukuchukia, ndio kama waume zenu, mkiwaweka karibu watakuwa marafiki kabisa.

NDOA TAMU jamani asikwambie mtu, tusifikiri ndoa inaweza kuvunjika kwa urahisi. Sometimes mkikosana, jaribu kukumbuka mmetokea wapi?? Kumbuka siku yako ya harusi, kumbuka mapenzi mliyo kuwanayo kipindi kileeee, halafu uya apply kwenye ndoa yako sasa.

Ndoa ina heshima yake kama mtaheshimiana, na hata kama mtapishana basi mmoja lazima akubali kushuka, ukijishusha mwanamke hutoonekana mjinga kama wengi mnavyofikiria, bali utaonekana mke mwenye busara asiyetaka kuibomoa nyumba yake kwa mikono yake, KUJISHUSHA ni dawa moja nzuri sana,  hata kama hujakosea, kwani ukikaa kimya au kama unamueleza ukweli yeye haelewi, no need kupigizana kelele weeeee, NI KUJISHUSHA TU ndio dawa pekeee.


MWISHO

No comments:

Post a Comment